Manny Pacquiao Aanza Kumpika Mwanaye, Mkewe Atokwa Machozi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Bingwa wa dunia wa masumbwi anayetajwa kuwa bondia bora wa muda wote, ameanza kumpika mwanaye Jimuel anayetaka kuingia rasmi ulingoni.

Jimuel mwenye umri wa miaka 18 ameanza rasmi mafunzo ya mchezo huo huku wazazi wake wakimsihi kuachana nao kutokana na namna ambavyo ni hatari kwa maisha ya wachezaji.

Pacquiao amelazimika kuanza kumpa mafunzo hayo baada ya Jimuel kusisitiza kuwa anaupenda mchezo huo kutoka ndani ya nafsi yake.

Mke wa Pacquiao, Jinkees ameeleza kuwa alitokwa machozi baada ya kusikia mwanaye ameamua kuingia kwenye mchezo wa masumbwi na hata kuanza kushiriki ngumi za ridhaa (armature), akishinda pambano lake la kwanza.

“Nilipokuwa nawaangalia, nilitokwa machozi. Mwanangu anataka kweli kuwa bondia. Nilimwambia mwanangu acha ni mchezo hatari, baba yako aliingia huko kwa sababu ya umasikini tu, lakini alisisitiza anataka kucheza kama baba yake,” Jinkees ameandika kwenye Instagram akiambatisha na picha ya Pacquiao akimfua Jimuel.

Pacquiao ambaye sasa ana umri wa miaka 40, hivi karibuni alishinda pambano lake la 70 dhidi ya bondia machachari kijana, Adrian Broner. Mwanaye anataka kuwa na uwezo wa kuiwakilisha nchi yake kama baba yake.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad