Mbunge CHADEMA Awalalamikia MA RC na Wakuu wa Wilaya Wanaowakamata Wananchi na Kuwaweka Ndani

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mbunge CHADEMA Awalalamikia MA RC na Wakuu wa Wilaya Wanaowakamata Wananchi na Kuwaweka Ndani
Mbunge wa Rombo (CHADEMA)  Joseph Selesini   amewalalamikia baadhi ya viongozi wa Serikali wakiwamo wakuu wa mikoa na wilaya kufanya vitendo aalivyoviita vya ovyo kwa wananchi.

Akiuliza swali bungeni leo, Selasini amesema anatambua juhudi mbalimbali ambazo zimekuwa zikifanywa na Serikali katika kutatua tatizo hilo.

Hata hivyo, amesema mkuu wa wilaya ya Hai amekuwa akiendelea na vitendo alivyoviita vya ovyo vya kuwakamata wawekezaji na wananchi pamoja na kushinikiza baadhi ya wanasiasa kwa kutumia askari wahame kwenye vyama vyao.

Hivyo, akahoji ni hatua gani zinachukuliwa na  Serikali kukomesha jambo hilo.

Akijibu swali hilo , Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Suleiman Jafo amesema ni kweli awali hali ilikuwa ni  mbaya kwa sababu idadi ya waliokuwa wanafanya vitendo hivyo ilikuwa ni kubwa.

“Wakuu wa mikoa, wilaya na wakurugenzi hasa wakuu wa wilaya walikuwa wakifanya mambo yasivyo lakini tunajua sisi ndani tumefanya tathimini hali imebadilika sana,” amesema.

Jafo amesema bado kuna baadhi ya kesi wanaendelea kushughulikia na hata mambo wanayozungumza (wabunge) mengine yapo katika utaratibu wa kuyashughulikia.

“Tuvute subira si kila kitu kukitangaze public  lengo letu ni utii wa sheria bila shurti kwa wananchi wote lakini kanuni na sheria kwa viongozi wote lazima zifuatwe,” amesema.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad