AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
TP mazembe walitua katika Uwanja wa Ndege wa Songwe kabla ya kuwasili Dar es salaam, ambapo imeelezwa kuwa walitua kwaajili ya kufanya matengenezo madogo.
Baada ya kutua Dar es salaam, wachezaji na viongozi walipokelewa na mashabiki wao waliojitokeza, ambao muda wote walikuwa wakiimba nyimbo za Kikongo na Kifaransa. Shangwe lao liliongezeka zaidi baada ya kumuona mshambuliaji hatari wa klabu hiyo, Tresor Mputu ambaye ana mabao manne mpaka sasa katika Klabu Bingwa Ulaya.
Inaelezwa kuwa baada ya kutua, Mazembe waligomea basi kubwa lililoandaliwa na wenyeji klabu ya Simba, bali walitumia mabasi madogo mawili na basi waliloandaliwa lilitumiwa na mashabiki wao.
Wakati huo huo wenyeji wa mchezo, klabu ya Simba wameianza safari asubuhi ya leo kurejea Dar es salaam kutoka mjini Morogoro, kufuatia mchezo wao kuahirishwa Jumatano, April 3 baada ya mvua kubwa kunyesha na kusababisha uwanja wa Jamhuri kujaa maji.
Mchezo huo wa Klabu Bingwa Afrika baina ya Simba na TP Mazembe utapigwa Jumamosi, April 6 katika Uwanja wa Taifa saa 10 jioni.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK