AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Akizungumza na waandishi habari Mjini Tabora Mwanri amedai suala hilo, lilipata tafsiri potofu kwa baadhi ya watu hasa kupitia mitandao ya kijamii.
"Nilichokuwa nalenga pale ni hiki hapa mfano nitoe kwenu kwa waandishi wa habari mara nyingi mnatuunga mkono Serikali katika kuleta maendeleo ya Tabora, inafika mahali katika kuzungumza na waandishi wa habari nawaambia uwezo wa kushukuru sina, nitachofanya kumuomba mwenyezi Mungu awashukuru kwa kazi nzuri mnayofanya." amesema Mwanri
Mwanri ameongeza kuwa "mimi nimekuwa nikiwaambia hata wananchi kuwa mimi siwezi kuwashukuru bali nitamwachia Mungu awashukuru, ila nilichosema siku ile ni nilimaanisha Rais Magufuli anafanya kazi nzuri na ni mambo makubwa yaliyotufurahisha mioyo yetu, ninachoweza kusema na kufanya ni kumuomba Mungu atusaidie kumshukuru Rais Magufuli, japo jambo lile lilipata tafsiri potofu"
"Ila nilichojifunza inapopelekwa habari kama ile masikio yanayopokea ni mengi usifikiri hata kama uko sawa ukafikiri utapokea kwa hisia hivyohivyo, kama masikio mengi yalipokea jambo hilo kwa tofauti sina cha zaidi ya kuomba msamaha kwa sababu nimeshafafanua na mimi ambao walininukuu vibaya natangaza nimeshawasamehe, ni Mungu peke yake hakuna binadamu atakayeweza kuchukua nafasi ya Mungu, nitakuwa nimechuja sana nikiamini binadamu anaweza kuchukua nafasi ya Mungu" amesema Mwanri
Mwanzoni mwa mwezi Aprili Mkuu wa huyo wa Mkoa alikaririwa na baadhi ya vyombo vya habari nchini juu ya kutoa kauli ambayo alieleza kuwa anamuomba Mungu amshukuru Rais Magufuli hali iliyomfanya kuzua taharuki kwenye mitandao ya kijamii.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK