Baada ya Kaachiwa kwa Dhamana Nyarandu Asimulia Yaliyomkuta

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Waziri Mstaafu wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu na Wenzake wamedhaminiwa na Wadhamini 2 huku yeye akidhaminiwa na Wadhamini 3, kila mmoja Tsh. Milioni 5.

Wanatakiwa kuripoti Kituo cha Polisi, Singida Mjini kesho saa 3

Akizungumzia tukio hilo, Nyalandu amesema alikamatwa jana saa 8 mchana akiwa kwenye kikao cha ndani na vijana 29 katika kijiji cha Itaja jimbo la Singida Kaskazini.

Amesema walivamiwa na watu walioanza kuuliza alipo Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Singida, Shaban Lyimo ambaye alisimama na kuwaeleza watu hao kuwa walikuwa katika kikao cha ndani cha Chadema.

“Kwanza walituliza kibali (cha kikao),  Lyimo akawajibu kuwa hatuna na ni kikao cha ndani hakihitaji kibali. Wakasema kuwa wao wametoka Takukuru Mkoa wanawahitaji watu wakaninyooshea kidole mimi (Nyalandu) na David Jumbe pamoja na mwenyekiti (Lyimo),” amesema Nyalandu.

Amesema walielezwa kuwa wanahitajika kwa ajili ya mahojiano Singida mjini  na walipofika wakaelezwa kuwa wanafuatilia masuala ya rushwa.

“Tulipofika polisi tulihojiwa zaidi ya masaa mawili  tukapewa dhamana ilikuwa imefika saa 4 usiku tuliambiwa kwamba twende kisha turudi asubuhi (leo), wakati tukijiandaa kuondoka, mkuu wa kile kituo akapigiwa simu na kutakiwa kufuta dhamana zetu, hivyo tukalala ndani hadi leo.”
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad