Jeshi la Somalia laua magaidi 18 wa al Shabaab

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kamanda wa vikosi vya Jubaland huko Jamame, Mural Ahmed Farah amewaambia wanahabari kuwa vikosi maalumu vya Somalia, vinavyojulikana kama Danab, na vikosi vya Jubaland vikisaidiwa na washirika wa kimataifa vimewaua magaidi hao baada ya kupokea taarifa kuhusu maficho yao. Ameongeza kuwa sita kati ya waliouawa kwenye operesheni hiyo ni wataalamu wa mabomu.

Oparesheni hiyo ya Jumatano imekuja kabla hata ya kupita siku mbili baada ya vikosi vya Somalia kuwaua magaidi 11 wa al Shabaab kwenye mapigano yaliyotokea mkoa wa Shabelle ya kati kusini mwa Somalia.

Wakati huohuo vikosi vya usalama vya Somalia vimewakamata magaidi  wanne kwenye opresheni iliyofanywa Weydow.

Wanajeshi wa serikali ya Somalia wakishirikiana na askari wa kikosi cha Umoja wa Afrika maarufu kama AMISOM wameimarisha vita dhidi ya magaidi wakufurishaji wa al-Shabab katika maeneo ya kati na kusini mwa Somalia ambapo wamefanikiwa kuwaangamiza magaidi wengi.

Somalia ilitumbukia katika vita vya wenyewe kwa wenyewe mwaka 1992 na katika miaka ya hivi hivi karibuni nchi hiyo imeshuhudia kushadidi hujuma za magaidi wakufurishaji wa Al Shabab na hivyo kuwasababishia raia wa nchi hiyo matatizo makubwa.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad