AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Lipuli FC itakutana na Azam FC kesho Jumamosi mkoani Lindi kwenye Uwanja wa Ilulu ikiwa ni siku chache baada ya kumaliza Ligi Kuu Bara msimu wa 2018/19.
Akizungumza na Championi Ijumaa, Matola alisema kuwa wana wakati mgumu wa kuwafunga Azam FC kutokana na wachezaji wake kuchoka kutokana na kutumia muda mwingi safarini.
“Tunajipanga lakini ratiba inatubana mechi ya mwisho tumecheza Mbeya tumetumia siku mbili njiani hadi kufika Lindi, tunapata siku moja tu ya kupumzika, hivyo hatuwezi kufanya vyema.
“Tuliwaomba TFF watusogezee mbele mechi hiyo lakini imeshindikana na tumewaomba basi wasogeze nyuma mechi ya ligi imeshindikana kwa hiyo hatuna jinsi, tunajipanga kwa hali ilivyo kwani ratiba haipo vizuri.
“Kwa kweli sisi ni binadamu na si mashine ukizingatia tunasafiri siku mbili njiani kisha tunapewa siku moja tu ya kupumzika, siyo vizuri tulihitaji muda zaidi wa kupumzika hasa ukizingatia tunatumia usafiri wa basi, tunaenda kucheza tu hivyo hivyo,” alisema Matola.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK