Mganga Mkuu: Watu 1,901 Wakutwa na Homa ya Dengue

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

MGANGA Mkuu wa Serikali, Prof. Mohamed Kambi,  amesema kuanzia Januari hadi Mei 2019, watu 1,901 wamepimwa na kuthibitika kuwa wana homa ya Dengue, miongoni mwao, 1,809 wanatoka jijini Dar es Salaam, Tanga 89,  ambapo mikoa ya Singida, Kilimanjaro na Pwani kila mmoja una mgonjwa mmoja.



Amesema hayo leo Alhamisi, Mei 16, 2019 wakati akizungumza na wanahabari jijini Dar es salaam na kuongeza kuwa wagonjwa ikoani Singida, Kilimanjaro na Pwani wote walitokea Mkoa wa Dar es Salaam na waligunduliwa na ugonjwa huo baada ya kufika kwenye mikoa hiyo.



Aidha, hakuna vifo zaidi vilivyoripotiwa sasa mbali na viwili vilivyoripotiwa awali mwezi huu wa Mei huku akiwataka wananchi kuchukua tahadhari na endapo wataona dalili zilizoainishwa kuhusu ugonjwa huo, wawahi katika vituo vya afya kwa vipimo na matibabu.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad