Mkapa Nae Afunguka Makubwa Kuhusu Mengi aeleza alivyosaidiwa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Rais mstaafu wa awamu ya tatu, Dkt. Benjamin Mkapa ameeleza masikitiko yake kufuatia msiba wa aliyekuwa Mwenyekiti wa makampuni ya IPP, Dr. Reginald Mengi kilichotokea Mei 2, huko Dubai.

Kupitia taarifa iliyotolewa na Ofisi yake, Mkapa ameeleza mchango wa Dr. Mengi katika maendeleo ya taifa wakati wa uongozi wake.

“Wakati wa urais wangu, Dr. Mengi kupitia shughuli mbalimbali alinifanya niwe Rais mzuri. Alikuwa mkweli katika maoni yake hata kama yalikuwa tofauti na misimamo yangu lakini hilo lilinifanya kufaidika na busara zake,” alisema Rais huyo mstaafu.

Aidha Mkapa aliyeongoza nchi kuanzia mwaka 1995 hadi 2005, ameongeza kuwa, utumishi wa Mengi katika sekta binafsi umeendelea kuwa muhimu hadi leo na anatambulika kama mtu aliyemshawishi kila anayetamani kuona nchi ikiendelea.

Alisema namna pekee ya kumuenzi ni kufuata njia na mifano aliyoionyesha, kwamba kupambana na umasikini siyo jukumu la Serikali peke yake bali ni la kila mtu.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad