AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Hayo yameelezwa ikiwa ni wiki ya pili tangu walipovunjiwa vibanda vyao na kuamrishwa na Mkuu wa Wilaya kuhamia katika eneo maalum lililotengwa.
Wakizungumza na www.eatv.tv, baadhi ya wafanyabiashara hao wamesema kuwa wamiliki wa maduka Mwenge wamekuwa wakiwahujumu kwa muda mrefu kwa kutoa rushwa kiasi cha kupelekea maafisa wa TANROADS kuharakisha uvunjwaji wa vibanda hivyo, ili waondoke.
Mjasiriamali, Deodatus Masili Bilanga amesema, "mwanzo wa kuvunjwa kwa vibanda hivi, Serikali ya mtaa haikuhusishwa kwa sababu hawajaja kwetu sisi kama watu wao kutuambia kuwa kuna suala kama hili. Uongozi wetu wa soko umevunjwa na kuvunjwa kwake kuna mazingira fulani, kwa sababu walikuwa imara hadi kwa mkuu wa mkoa walikuwa wanafika, lakini wakakutana na kashikashi nyingi hadi panavunjwa hapa walikuwa wamewekwa ndani."
Kwa mujibu wa wajasiriamali hao, baada ya Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Mh.Daniel Chongolo kuvunja uongozi wa soko hilo, hawana msemaji yeyote wa matatizo yao na sehemu waliyopelekwa haina mahitaji muhimu kama maji na vyoo, hali inayopelekea kuwepo kwa hatari ya mlipuko wa magonjwa kama Kipindupindu.
Naye mjasiriamali anayejihusisha na biashara ya mihogo, Bi Joyce Yoyo mkazi wa Goba amesema alikuwa na kibanda chake lakini kimebomolewa, hali inayompelekea kufanya biashara juani na kwamba wafanyabiashara wengi wanashindwa kwenda mahali walikoelekezwa kwa sababu ni sehemu ambayo imekaa pembeni na hakuna watu wengi.
Kwa upande wake, ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni kupitia kwa msaidizi wake, amesema kuwa ardhi ni mali ya serikali na wafanyabiashara wamepangiwa mahali pa kwenda, hawapaswi kuhoji maamuzi hayo.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK