Spika Ashangazwa Ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo Kusimama...Ataka Serikali Kufafanua

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Spika Job Ndugai ameitaka Serikali itakapo kuwa inahitimisha mjadala wa bajeti ya Wizara ya Ujenzi, kueleza kwa nini ujenzi wa mradi wa Bandari ya Bagamoyo mkoani Pwani haufanyiki licha ya mzabuni kupatikana kutoka nchini China.

Amehoji hivyo, leo Bungeni baada ya Wabunge mbalimbali kuhoji mradi huo wa bandari kukwama wakati wakichangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano ya mwaka 2019/20.

Amesema kuna wakati alitembelea China na walisema ujenzi wa bandari hiyo ukikamilika utakuwa na tija kubwa kwa nchi kuliko ujenzi wa reli ya kisasa (Standard Gauge Railway - SGR) unaojengwa, na kushangaa kuwa ujenzi wa reli umeanza badala ya bandari.

Amefafanua kuwa kukamilika kwa SGR bila kuwa na bandari ya kisasa kama hiyo ambayo ilikuwa ijengwe Bagamoyo ni kazi bure kwani mpaka sasa nchini hakuna bandari nzuri hivyo Serikali inapaswa kuliona hili.

Aidha, baadhi ya Wabunge waliohoji kuhusu suala hilo na kuhitaji ufafanuzi ni Hussein Bashe(Nzega Mjini-CCM), Lucy Magereli(Viti Maalum-CHADEMA), Ally Salehe(Malindi-CUF), Charles Tizeba (Buchosa-CCM) na Dkt. Shukuru Kawambwa(Bagamoyo-CCM).

Mwananchi
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad