Abiria Afariki Katika KITUO Cha Basi Ubungo

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Abiria mmoja aliyetambulika kwa majina ya Mwanaidi Said (83), aliyekuwa anasafiri kutoka Dar Es Salaaam kwenda mkoani Tabora, amefariki dunia jana alfajiri katika kituo cha mabasi cha Ubungo akiwa ndani ya  basi kabla ya kuanza kwa safari.



Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, Kamanda wa Polisi mkoa wa Kipolisi, Kinondoni, Mussa Taibu amesema kuwa abiria huyo amekutwa na mauti akiwa amekaa kwenye kiti cha basi hilo linalofanya safari zake kati ya Dar es Salaam na Kigoma kupitia mkoani Tabora.

Kamanda Taibu amesema Msafiri huyo “Alikuwa akisumbuliwa na saratani na alikuwa anakwenda mkoani Tabora baada ya kumaliza matibabu yake hapa Dar es Salaam na vyeti vimeonyesha hivyo,“.

Kwa mujibu wa maelezo ya mtoto wa mama huyo aliyekuwa ameambatana naye kwenye safari hiyo, Faida Paul amesema kuwa mazishi ya mama yake yamefanyika jana Kigamboni.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad