Kiingereza Kuendelea Kuwa Lugha ya Kufundishia - Waziri Ndalichako

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce amesema Kiingereza kitaendelea kuwa lugha ya kufundishia na kujifunzia katika ngazi ya elimu ya sekondari, vyuo vya kati na vyuo vikuu.

Akijibu swali la mbunge wa Tabora Kaskazini (CCM), Athuman Maige leo, Ndalichako amesema Kiingereza kitaendelea kutumika kwa sababu ya umuhimu wake kitaifa, kikanda na kimataifa kwa mawasiliano na biashara ili kuwajengea wanafunzi ufahamu na umahiri wa lugha hiyo.

“Suala la matumizi ya lugha ya kufundishia na kujifunzia ni la kisheria kama ambavyo sheria ya elimu sura 353 inavyoelekeza. Sheria hiyo inabainisha matumizi ya lugha mbili za kufundishia na kujifunzia ambazo ni Kiswahili na Kiingereza.”

“Kwa sasa Kiswahili kinatumika kufundishia katika ngazi ya elimu ya awali na msingi, vyuo vya ualimu ngazi ya cheti na vyuo vya ufundi stadi,” amesema Profesa Ndalichako.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Hii inaleta Faraja Sana.
    Ukitaka kujua umuhimu Mwangalie Shish Baby anavyo I Anya na kwa shauku kubwa anavyo isema you know what awm seiying. Tuanzie toka darasa LA uchekechea.

    ReplyDelete

Top Post Ad