Jeshi la Sudan ‘lakubali yaishe’, wananchi washerehekea

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Hatimaye viongozi wa jeshi la Sudan leo wamekubaliana na viongozi wa umoja wa vyama vya upinzani kuchangia madaraka hadi uchaguzi mwingine wa kidemokrasia utakapofanyika.

Pande hizo mbili zimekubaliana kuwa na wawakilishi katika ngazi zote za juu za Serikali kwa kipindi kisichopungua miaka mitatu.

Pia, wamekubaliana kuunda Serikali inayowahusisha wataalam na wanazuoni ambayo itaanza kwa kufanya uchunguzi wa vurugu zilizokuwa zimejitokeza katika kipindi cha wiki za hivi karibuni.

Taarifa za makubaliano hayo zimeamsha shamrashamra kwa wananchi katika mitaa ya majiji na miji ya nchi hiyo, kwa mujibu wa Aljazeera.

“Tunatumaini kuwa huu utakuwa mwanzo mzuri kwa ajili ya faida ya Wasudan wote,” alisema Kiongozi wa chama cha upinzani cha Forces for Freedom and Change (FFC), Omar al-Degair.

Naye kiongozi wa Baraza la Mpito la Jeshi, Jenerali Mohamed Hamdan Dagalo alisema, “makubaliano haya yatawahusisha watu wote, hakuna hata mmoja ambaye atatengwa. Tunawashukuru viongozi mbalimbali wa Afrika hususan Ethiopia kwa juhudi zao pamoja na uvumilivu wao katika kuhakikisha tunafika hapa.”

Awali, Jeshi la nchi hiyo lilikuwa na kigugumizi kuhusu kuruhusu viongozi wa umoja wa vyama vya upinzani kuunda Serikali ya kiraia. Walisema nchi hiyo itaongozwa na viongozi wa kijeshi kwa kipindi cha miaka mitatu wakati wanafanya maandalizi ya uchaguzi mkuu.

Sudan imekuwa katika vurugu tangu Jeshi la nchi hiyo lilipomuondoa madarakani aliyekuwa rais, Omar al-Bashir.

Bashir aliiongoza Sudan tangu Juni, 1989 alipofanikiwa kuipindua Serikali iliyokuwa madarakani. Mwaka huu, wananchi walianzisha maandamano makubwa ya kupinga utawala wake na kusababisha jeshi kumuondoa madarakani.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad