Mama KANUMBA Amkana Baba Kanumba Mchana Kweupe..Adai Alikuwa tu Mchepuko Wake

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


MAMA wa aliyekuwa staa wa Bongo Movie, marehemu Steven Kanumba, Bi. Flora Mtegoa, amesema hakuwahi kuolewa na baba wa mtoto wake huyo (mzee Charles Kanumba) badala yake alikuwa mchepuko wake tu kwani tayari baba huyo alikuwa na mkewe na watoto.



Bi. Flora amesema hayo jana Jumatatu wakati akipiga stori ndani ya kipindi cha Kata Mbuga cha +255 Global Radio na kusema kuwa mzee huyo hakuwahi kuwa na mawasiliano wala kumhudumia mtoto huyo mpaka umauti ulipomfika, lakini Baba Kanumba amekuwa msitari wa mbele kudai mali za marehemu Kanumba jambo ambalo mama huyo amepingana nalo vikali.



Kuhusu mali alizoacha Kanumba

“Huwa nina-miss vingi sana kutoka kwa mwanangu, uwepo wake, upendo wake, waliojifanya ni marafiki zake leo wala huwaoni. Naishukuru serikali baada ya miaka saba ya kifo chake, mikataba ya Kanumba na mzee Majuto imerudiwa. Nilikuwa nalia nikikuta muvi za mwanangu zikichezwa. Namshukuru Rais Magufuli na Waziri wa Sanaa, Dkt. Mwakyembe wamenifuta machozi.



“Nilikuwa sitegemei kupata chochote kutoka kwenye muvi za Kanumba, nilichopewa na Steps (Entertainment) nasema asante na bado niko nao bega kwa bega, tunafanya vitu vingi, siwadai wala hawaniadi.



Kuhusu Baba Kanumba

“Baba Kanumba hajawahi kuja kwenye msiba wa Kanumba, mwanangu alipokufa walimtumia tiketi ya ndege, wakamtumia gari kutoka kwake Shinyanga mpaka Mwanza Airport, hakuwahi kuja, mpaka leo hajawahi kuja, lakini anaposikia kuna pesa anataka kuja, sasa ana uhakika kama Kanumba alikufa?



“Inawezekana sio baba mzazi wa Kanumba, kwa sababu tangu Kanumba alipokuja Dar, hakuwahi kuja kumtembelea wala kujua anaishi wapi, hata kuwasiliana naye, sasa anasubiri kwenye faida, hili nasema liwe fundisho kwa akina baba wanotelekeza watoto.


“Kwa bahati mbaya sikuwahi kuwa na mawasiliano naye, nimekaa Shinyanga miaka 22, Kanumba amesoma pale Shinyanga lakini baba huyu hakuwahi kuwasiliana naye. Akahamia Dar es Salaam, hakuna mawasiliano naye, mpaka amekufa hadi leo hajui hata kaburi lake lilipo.


“Kanumba aliwahi kukaa kwa baba yake kwa miezi tisa, alipotoka huko hakutaka kurudi tena kule. Mzee huyu hakuwahi kunisaidia kwa chochote na nilimwambia apige hesabu ya pesa zake alizowahi kumsaidia huyo mtoto, kama ikifika hata jero namrudishia.

“Mimi nilikuwa mchepuko, sikuwa mke wake, hata mawifi zangu sikuwahi kuwajua, alikuwa na mke wake, na watoto wake. Kwa hiyo aliponipa ujauzito akaiacha, labda alimuogopa mkewe, na mimi kwa sababu nilikuwa nimetoka kuachana na mume wangu wa ndoa, nikasema ndo wanaume walewale. Shinyanga nafahamika kama mama Kajumulo.

“Kanumba hakuwahi kufahamika kwenye familia, hakuwahi kulipiwa mahali ili ahalalishwe kwenye ukoo kama yeye ni Msukuma kwa mila za Kisukuma, wala hakuwahi kuitwa kwenye familia. Kanumba ndo alimtafuta baba wala sio baba alimtafuta Kanumba,” alisisitiza mama huyo.

GPL
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. sasa njo nini? baba wa mtoto wako huyo, hauna ata aibu

    ReplyDelete

Top Post Ad