Wanawake 11 Wakamatwa Kwa Kurekodi VIDEO za Ngono

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Jeshi la Polisi nchini Kenya linawashikilia wanawake 11 kwa tuhuma za kurekodi filamu za ngono na kuziuza.

Kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa na Citizen, mbali na wanawake hao, polisi pia wamewakamata watu wawili waliotajwa kwa majina ya Merceline Atieno na Enock Ochieng wanaodaiwa kuwa wanamiliki tovuti yenye maudhui ya ngono ya kulipia kwa kushirikiana na kampuni ya Multi Meida Illc.

Watu hao wawili wanadaiwa kuwa ndio wanaowasimamia wanawake hao katika kukamilisha biashara hiyo haramu.

Polisi wameeleza kuwa watu hao walikamatwa baada ya askari kupata taarifa na kuvamia nyumba waliyokuwemo. Imeelezwa kuwa katika nyumba hiyo, polisi walikamata kompyuta mpakato 16, kamera kadhaa, simu za mkononi, flash na midoli ya ngono.

Watuhumiwa hao walifikishwa mahakamani Ijumaa, Julai 12, 2019 na kusomewa mashtaka yao mbele ya Hakimu Mkuu, Florence Macharia lakini hawakutakiwa kujibu chochote.

Polisi waliiomba mahakama kuwapa siku tano ili kukamilisha upelelezi, ombi ambalo Mahakama ililiridhia.

Kama ilivyo kwa Tanzania, nchini Kenya ni kosa la jinai kwa mtu kurekodi, kuchapisha, kusambaza picha zenye maudhui ya ngono (pornography) au hata kujihusisha na biashara hiyo na sheria imetaja adhabu kali kwa watakaokutwa na hatia.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad