Mjumbe wa NEC atolewa povu kumlazimisha askari kusalimia kwa salamu ya CCM

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Wadau na wanasiasa wamemjia juu Mjumbe wa Halmashauri Kuu Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Pwani Haji Abuu Jumaa baada ya kumlazimisha askari polisi Koplo Said kusalimia kwa salamu ya CCM wakati alipomwagiza kutoa ufafanuzi juu ya masuala ya ulinzi na usalama katika kata ya Vianzi, wilani Mkuranga mkoani Pwani.

Katika video fupi ambayo inatembea mtandaoni mjumbe huyo wa NEC, Pwani anaonekana kumlazimisha askari huyo na pale alipokataa alimwamuru aondoke na maelezo hayo kutolewa na mtendaji wa kata hiyo.

Katika kumlazimisha kwake, Haji Jumaa alitumia mifano ya mabosi wa askari huyo akiwemo Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola ambaye hutembea na ilani ya CCM pamoja na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha ambaye amewahi kunukuliwa akisalimia kwa kutumia salamu ya CCM.

Askari huyo alikataa na kutoa maelezo kwamba askari hapaswi kuwa na chama chochote cha siasa kwani analinda raia wa vyama vyote.

Kufuatia tukio hilo Maria Sarungi ambaye ni moja ya wanaharakati wa masuala ya haki za binadamu amesema:
“Hivi CCM mnaona sawa kabisa kada wenu kuvunja sheria? Ina maana mpaka leo CCM haielewi miiko ya utumishi wa umma? Enzi ya chama kushika hatamu imekwiisha! Sheria inamkataza polisi kuwa na ushabiki. Wanaofanya hivyo wanakiuka miiko na sheria.”

Naaye Mbunge wa Tarime Vijijini kupitia Chadema John Heche kupitia Twatter yake ameandika: “Tumefika hapa kwasababu wakuu wa jeshi la polisi wametaka iwe hivyo, inakuaje katika karne hii eti kiongozi wa chama fulani cha siasa anaita askari polisi na kumwambia mambo kama haya huyu ni moja walau ameonesha kutotii ujinga, wangapi wanatii mambo mengi ambayo hayaonekani!!



----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad