Uongozi wa 2 FACE wazungumzia afya yake, kukimbizwa hospitalini

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Taarifa zilizosambaa mitandaoni wiki hii kuhusu hali tete ya kiafya ya mwanamuziki wa Nigeria, 2Face Idibia ambaye sasa anajiita 2Baba zimeuibua uongozi wake na kuweka mambo sawa.

Kulikuwa na taarifa kuwa msanii huyo alikuwa katika hali mbaya na amelazwa hospitalini. Taarifa hizo ziliendelea kudai kuwa 2Baba alihudhuria mkutano na waandishi wa habari kwa ajili ya kutimiza masharti ya mkataba wake na ‘Nigerian Stock Exchange’.

“Alitoka hospitalini kuhudhuria mkutano kwa sababu za kuhakikisha anakidhi vigezo vya mkataba wake, lakini alikimbizwa tena hospitalini baada tu ya kumaliza mkutano na waandishi wa habari,” taarifa hiyo ilieleza.

Hata hivyo, chombo cha habari cha E-Day cha Nigeria kilizungumza na uongozi wa mkali huyo wa ‘African Queen’ na ulikanusha taarifa hizo.

Kwa mujibu wa E-Day, mmoja wa viongozi wa 2Baba alieleza kuwa msanii huyo yuko katika hali nzuri ya kiafya na hajawahi kulazwa hospitalini hivi karibuni.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad