Wanaosambaza picha za marehemu katika mitandao kuchukuliwa hatua

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni amelitaka Jeshi la Polisi nchini kuwakamata na kuwachukulia sheria wale wote wanaosambaza picha za marehemu katika mitandao ya kijamii kwani kufanya hivyo nikosa kisheria

Masauni ametoa kauli hiyo Mjini Morogoro ambapo amesema kuwa kusambaza picha za marehemu katika mitandao ya kijamii ni kuwadhalilisha wahusika na ni uvunjaji wa sheria za nchi.

“Ninaziagiza mamlaka na vyombo vinavyohusika vihakikishe vinafuatilia na kuchukua hatua kwa wale ambao wanakiuka sheria za nchi yetu kwa kusambaza mitandaoni picha za marehemu,” aliagiza Masauni.

Aidha Masauni amesema siyo vema kuanza kutumia majanga ya Kitaifa kama ajali ya moto iliyotokea Mkoani Morogoro na kusababisha watu zaidi ya 70 kufariki dunia ndani ya muda mfupi hivyo kuanza kusambaza picha za waathirika mitandaoni kwa dhamira ya kudhalilisha sio jambo la busara.

“Watu hawa wamefariki dunia na mtu yeyote katika tukio lile angekufa, mimi au wewe, ndugu yako au jamaa yako, fikiria kama ni jambo limekukuta au ndugu yako halafu ukachukua picha na kuisambaza kwenye mitandao, katika mazingira kama yale,” Masauni alisema.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad