AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Goodluck Gozbert ni Mwimbaji wa nyimbo za Injili, ambaye ametamba na nyimbo nyingi mpaka sasa kama Shukrani, Hauwezi Kushindana, Hao Hao, Ipo Siku na sasa Nibadilishe' wimbo ambao una wiki mbili tangu utoke.
Akizungumza na EATV & EA Radio Digital kuhusu namna ya muziki wake unavyozungumziwa na watu mbalimbali kwamba hauendani na mahadhi ya kuwa nyimbo za Injili, Goodluck anasema kwake hana cha kusema na huwa anaacha hivyo hivyo.
"Sio kila Mwimbaji anaimba nyimbo za Injili hata kama anaitwa mwimbaji wa nyimbo za Injili, maana ukizungumza nyimbo za dini ni nyimbo zinazohusu dini fulani na nyimbo za Injili ni nyimbo zote zinazo ongelea habari zote ziletazo wokovu," aliongeza.
Goodluck ameendelea kueleza kuwa, kuna waimbaji wanaimba nyimbo za Injili lakini wao wana muabudu Mungu tu na wengine wanamsifu Mungu peke yake hivyo tupo tofauti lakini wote huwa tunaitwa waimbaji wa nyimbo za Injili nayo ni sawa," aliongeza zaidi.
Pia aliongeza mabadiliko ya Teknolojia yamewafanya na wao pia wabadilike lakini Injili ni ile ile na muziki wao pia upo vile vile.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK