Lukaku Ampiga Kijembe Ole, eti Conte ni kocha

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


MILAN, ITALIA. STRAIKA, Romelu Lukaku ni kama amempiga kijembe Ole Gunnar Solskjaer kiaina baada ya kumsifu kocha wa Inter Milan, Antonio Conte na kusema ndiye anayejua namna bora ya kumtumia.

Lukaku ameungana na Conte huko Inter Milan, baada ya jaribio la kumsajili alipokuwa Chelsea kukwama wakati straika huyo wa Kibelgiji alipoamua kwenda kujiunga na Manchester United iliyokuwa chini ya Jose Mourinho miaka miwili iliyopita.
Kwenye kikosi cha Inter chini ya Conte, Lukaku amekuwa kwenye ubora wake, akifunga kwenye Milan derby wakati timu yake ilipojipigia AC Milan 2-0, huku likiwa bao lake la tatu kwenye Serie A msimu huu.

Akizungumza baada ya mechi, Lukaku alisema: “Nimefurahishwa sana na matokeo haya, na pointi tatu hizo kwenye mechi hii spesho kabisa.

"Sasa, tunafikiria mechi ya Lazio, ambayo bila ni ngumu. Uhusiano wangu na Conte? Jamaa ni bonge la kocha kwa sababu anawasaidia wachezaji kukuza soka lao.
"Kwenye umri wangu wa miaka 26, nilihitaji kocha wa aina hii, mtu anayekuhamasisha kila siku. Ninafuraha kuwa hapa chini yake na kuvaa jezi za Inter.”

Maneno hayo ya Lukaku yanaonekana kama kijembe kwa Solskjaer, ambaye wala hakusita kumzuia asiondoke kwenye timu, akimfungulia mlango wa kutokea Man United akimuuza kwa Pauni 73 milioni na kuamua kubaki na washambuliaji Marcus Rashford na Anthony Martial na kinda Mason Greenwood kwenye kikosi chake cha Old Trafford. Lakini, Lukaku tangu atue Inter amekuwa moto, ameshafunga mabao matatu katika mechi tano.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad