AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
KLABU ya Yanga imewaonya Shirikisho la Soka nchini (TFF) kamwe isithubutu kuwalazimisha kuvaa jezi yenye nembo nyekundu ya mdhamini .
Hivi karibuni TFF iliingia mkataba na Kampuni ya simu ya Vodacom kudhamini Ligi Kuu Bara kwa udhamini wenye thamani ya Sh 9 bilioni.
Kampuni ya Vodacom inatumia nembo nyekundu kama utambulisho wao ambapo Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Fredrick Mwakalebela amesema wanasikia tu kuwa msimu huu lazima kila timu ivae jezi yenye nembo nyekundu lakini wao hawatakubali hilo.
"Tumesikia maneno mengi kuwa msimu huu lazima kila timu ivae jezi yenye nembo nyekundu ambayo ni ya mdhamini lakini hilo kwetu hatutakubali.
"Katiba ya Yanga ambayo imepitishwa na TFF, Baraza la Michezo la Taifa (BMT) na Msajili inatambua rangi tatu za Klabu, njano, kijani na nyeusi, hivyo hiyo rangi nyekundu hatuitambui"alisema Mwakalebela.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK