AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Hatua hiyo inafuatia kukamilika kwa kazi ya uchambuzi wa maombi ya mikopo yapatayo 55,444 ya wanafunzi ambao wamepata udahili katika taasisi mbalimbali za elimu ya juu nchini.
Akizungumza na wanahabari ofisini kwake jijini Dar es salaam leo (Jumatatu, Oktoba 14, 2019), Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB Abdul-Razaq Badru amesema wanafunzi watakaopangiwa mikopo wataweza kupata taarifa zao kupitia akaunti zao kwenye mtandao wa taasisi hiyo.
Pamoja na kutangaza orodha hiyo, Badru amesema HESLB pia imeamua kutoa fursa kwa waombaji 4,794 ambao bado hadi sasa hawajakamilisha maombi yao kukamilisha kwa kuambatisha nyaraka muhimu mtandaoni.
Kuhusu malengo ya mwaka huu wa masomo, Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB amesema Serikali imetenga TZS 450 bilioni ambazo zitawanufaisha jumla ya wanafunzi 128,285.
Kati yao, wanafunzi zaidi ya 45,000 watakuwa ni wa mwaka wa kwanza na wengine 83,285 ni wanufaika wa mikopo wanaoendelea na masomo. Bajeti ya mwaka wa masomo 2018/2019 ilikuwa TZS 427.5 bilioni na iliwanufaisha jumla ya wanafunzi 123,329
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK