Habinder Singh Seth Kaandika Barua Kwa DPP Kukiri Makosa Yake

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mfanyabiashara maarufu , Habinder Singh Seth ambaye anakabiliwa na mashtaka ya uhujumu uchumi ameandika barua kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kukiri makosa na kuomba msamaha.

Wakili wa Seth, Michaele Ngalo, ameiarifu Mahakama ya Hakimu Mkaazi Kisutu jijini Dar es Salaam leo Alhamisi Oktoba 10 mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shahidi wakati kesi hiyo ilipotajwa.

Seth pamoja na mfanyabiashara mwenzake James Rugemalira,  kwa pamoja wanakabiliwa na mashtaka 12 wanayodaiwa kuyatenda jijini Dar es Salaam, Afrika Kusini, Kenya na India.

Washtakiwa hao walifikishwa kwa mara ya kwanza katika Mahakama hiyo Juni 19, 2017 na hadi sasa upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika.

Miongoni mwa mashtaka hayo ni kula njama, kujihusisha mtandao wa uhalifu , kughushi na kutoa nyaraka za kughushi, kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu, kutakatisha fedha na kuisababisha serikali hasara ya Dola milioni 22 na Shilingi za Tanzania bilioni 309.

Wakili wa Serikali, Wankyo Simon amethibitisha kuwa wamepokea barua ya Seth wanaifanyia kazi na majibu yatatolewa.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Oktoba 24, 2019
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad