AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
RAIS John Magufuli amesema anajutia kwa kihelehela chake cha kujazafomu ya kugombea nafasi hiyo na amewaomba viongozi wa dini kumwombea kutoka na ugumu wa kazi alionayo
Magufuli amesema hayo leo Oktoba 4, 2019 wakati akiongea na wananchi wa mji Wa Mlowo mkoani Songwe kwenye ziara yake ya kikazi mkoani humo.
"Ndugu zangu kazi hii ni ngumu sana hata mawaziri wangu hawalali usingizi na hawajui kama kesho yake wataamka wakiwa katika nafasi zao," amesema.
Amesema kila unapoangalia kusonga mbele ujue kuna maadui sasa lazima tuchape kazi kwa kumtanguliza Mungu na wale waliojitoa ufahamu Mungu awasaidie.
"Eti mtu wa chama fulani anafurahia. ndege ya Tanzania kushikiliwa katika nchi nyingine, ninawaomba viongozi wa dini kubeba jukumu la kuliombea hilo," amesema Magufuli.
Pamoja na mambo mengine amesema serikali imetoa billion 18 kwa ajili ya ujenzi wa uwanja wa ndege wa kimataifa wa Songwe (SIA) na mkandarasi anaendelea na kazi, lengo likiwa ni kwa ndege kubwa kutua.
Vilevile rais Magufuli ameimiza upendo ,amani, ushirikiano kwa watanzania wote na kumtangyuliza Mungu kwa kila jambo.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK