Mahakama Kuu yatengua hukumu ya kifungo cha miezi mitano alichotumikia Mhe. Sugu

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mbeya leo tarehe 11 October 2019 imetengua Hukumu, Mwenendo na Kifungo alichohukumiwa Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi almaarufu Sugu kwa kile ambacho Mahahaka Kuu imeeleza kuwa ni ubatili wa mwenendo katika kesi hiyo.





Akisoma Uamuzi wa Rufaa hiyo Nambari 29 ya Mwaka 2018, Iliyowasilishwa na Sugu kupitia Mawakili Peter Kibatala na Faraji Mangula, Jaji Utamwa amesema kwamba kulikuwa na Makosa yasiyotibika katika mwenendo wa shauri hilo, Hasa pale ambapo aliyekuwa Hakimu Mwandamizi Mteite wa Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Mbeya aliposhindwa kuwasomea Mashtaka Washtakiwa katika hatua ya usikilizaji wa awali (Preliminary Hearing).

Katika Hukumu yake iliyosomwa na Naibu Msajili wa Mahakama wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya, Jaji Utamwa amesema kuwa hakubaliani na hoja za upande wa Serikali ambao ni ndio Wajibu Rufaa, Kwamba mapungufu hayo yanatibika.

Jaji Utamwa amesema kwamba makosa hayo yanaathiri mwenendo mzima wa kesi iliyopelekea kufungwa kwa Sugu na mwenzake Emmanuel Masonga.

Mwezi Februari mwaka huu, Mheshimiwa Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ na Katibu wa CHADEMA Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Emmanuel Masonga walihukumiwa kifungo cha miezi mitano na Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad