Lipuli Yazifunika Simba, Yanga SC

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Simba, Yanga SC Martha Mboma, Dar es Salaam KLABU ya Lipuli, imeweka rekodi kwa mara ya kwanza kuwa timu ambayo imefunga mabao mengi zaidi ya Simba na Yanga katika Ligi Kuu Bara.

Lipuli imefunga mabao 18 katika mechi 10 ambazo imecheza hadi sasa msimu huu kwenye Ligi Kuu Bara inayoshirikisha timu 20.



Timu hiyo kwenye mechi 10 ambazo imecheza, mechi tano imeshinda na kupoteza mbili tu, huku ikitoa sare tatu na kujikusanyia pointi 18. Kwenye msimamo inashika nafasi ya tatu nyuma ya vinara Simba na Kagera Sugar wanaoshika nafasi ya pili.



Simba ambayo mshambuliaji wake Meddie Kagere anaongoza kwa kufunga mabao akiwa nayo nane, yenyewe imefunga mabao 16 katika mechi tisa, huku Yanga ikifunga mabao sita katika mechi tano.



Kwa maana hiyo, Lipuli imeifunika Simba na Yanga ambazo ndizo zinaaminika kuwa na washambuliaji hatari zaidi na mara kadhaa wamekuwa wakiongoza kwa ufungaji. Ingawa ni mwanzoni tu mwa ligi lakini ni picha kuwa huko mbele mambo yatakuwa hatari zaidi.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad