AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
WATU tisa wa familia mbili, wakiwa ni wanawake wanne na watoto watano, wamefariki katika Kata ya Nyatukala wilayani Sengerema, mkoani Mwanza, baada ya nyumba zao kukumbwa na maji kutokana na mvua kubwa inayonyesha.
Mvua hiyo iliyoanza kunyesha majira ya asubuhi, ilisababisha maafa hayo kwa baadhi ya nyumba ambazo zipo pembezoni mwa mto ambapo pia daraja muhimu limekatika na kukwamisha mawasiliano na usafiri katika maeneo hayo.
Mkuu wa wilaya hiyo, Dkt. Emmanuel Kipole, amewataka wananchi wanaoishi katika maeneo hayo kuondoka na kwenda katika maeneo ya muda ambayo tayari serikali imeyabainisha ili kuepusha madhara zaidi.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanz,a John Mongella, ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa, amewataka wakazi wa maeneo hayo kuchukua tahadhari ili kuepusha kupoteza maisha ya wananchi wengine zaidi..
Miili yote imepatikana na imehifadhiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Sengerema, baada ya zoezi la uokoaji kufanywa na wananchi kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama kwa kutumia nyavu na kamba.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK