AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Hayo yamejiri baada ya kukubaliana na matokeo ya uchunguzi uliokuwa unafanywa na wachunguzi wa kimataifa juu ya mwenendo wa uchaguzi uliopita na kumfanya asalie madarakani.
Wachunguzi hao walitengua matokeo yaliyomtangaza Morales mshindi wakisema kulikuwa na udanganyifu katika upigaji wa kura mnamo mwezi Oktoba mwaka huu.
Licha ya kujiuzulu, Morales ametangaza nia ya kuitisha uchaguzi mpya na kuvunja tume ya uchaguzi ambayo ilikuwa awali.
Amenukuliwa akisema kuwa ameamua kuitisha uchaguzi mwingine ili Wananchi wa Bolivia waweze kuchagua Serikali mpya kwa njia ya Kidemokrasia.
Kwa wiki kadhaa sasa nchi ya Bilivia imeshuhudia machafuko na ghasia dhidi ya madai ya udanganyifu katika uchaguzi wa Oktoba 20, ambapo watu watatu wameuawa na zaidi ya 300 wamejeruhiwa.
Matokeo ya uchaguzi uliopita yalimpa ushindi Morales kwa asilimia 10 zaidi dhidi ya mpinzani wake Carlos Mesa na kupelekea upande wa upunzani kuishutumu Serikali kwa udanganyifu.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK