Yanga Kucheza na JKT Tanzania Leo

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

YANGA inarejea mzigoni kwenye Ligi Kuu Bara leo Ijumaa kwa kuikabili timu yenye fiziki nzuri ya JKT Tanzania inayonolewa na Kocha Abdallah Mohamed ‘Bares’.



Huo utakuwa mtihani mwingine kwa kocha wa muda wa Yanga, Charles Mkwasa ambae kuna uwezekano mkubwa akapewa nafasi hiyo mpaka msimu umalizike licha ya kwamba makocha kadhaa wanatajwa.



Bares amemwambia Mkwasa kwamba kikosi chake kipo tayari kwa mchezo wa kesho ndani ya Uwanja wa Uhuru na wanaiheshimu sana Yanga kwa vile wanaelewa presha waliyonayo.



“Hakuna ambaye haoni kwa sasa namna ushindani ulivyo, nimewapa majukumu wachezaji na wanayambua kwamba tunahitaji pointi tatu ili kuzidi kujiweka kwenye nafasi nzuri ya ushindani.



“Tunatambua aina ya timu tunayokutana nayo ni ngumu na ina wachezaji wenye uzoefu, hilo halitupi taabu kwani mpira ni dakika 90, tutapambana, mashabiki watupe sapoti,” alisema Bares.



JKT Tanzania ipo nafasi ya sita ikiwa imecheza mechi 10 na pointi zake 15, itamenyana na Yanga iliyo nafasi ya 15, imecheza mechi tano na ina pointi zake 10.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad