Yanga Wakabidhiwa Milioni 10 Baada ya Kuitungua Ndanda

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

TIMU ya Yanga imepokea kitita cha tsh milioni 10 kutoka kwa wadhamini wao, kampuni ya GSM ikiwa ni sehemu ya kuwapa motisha baada ya kuifunga Ndanda FC kwa bao 1-0 katika Uwanja wa Nangwanda Sijaona, jana Ijumaa, Novemba 8, 2019.



Patrick Sibomana ndiye aliibuka shujaa kwa kufunga bao moja la ushindi kwa Yanga dhidi ya Ndanda kwenye mchezo wa Ligi Kuu huku Yanga ikiwa chini ya Kaimu Kocha Mkuu, Boniface Mkwasa na msaidizi wake Said Maulid baada ya kumtimua Mwinyio Zahera.



Yanga iliwalazimu wasubiri mpaka dakika ya 75 kushinda mchezo huo mara baada ya Sibomana kupachika bao hilo kwa mpira wa adhabu akiwa nje kidogo ya 18 ambao ulizama jumla ndani ya nyavu za lango la Ndanda FC.



Ushindi huo unaifanya Yanga kufikisha jumla ya pointi 10 ikiwa imecheza mechi tano imeshinda mbili na imetoa sare tatu na kupoteza mchezo mmoja mbele ya Ruvu Shooting.



Kabla ya Mechi hiyo, GSM ilitoa ahadi ya kuipa Yanga Tsh milioni 10 endapo itashinda mechi hiyo na Wanakuchere, jambo ambalo Yanga wametekeleza hiyo kukabidhiwa zawadi hiyo.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad