Zari Adai Kuwa King Bae Wake Amekufa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


INADAIWA mitandaoni kwamba, kati ya wanawake wanaojua kupaniki, basi mwanamama Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ anaweza kuwa kwenye kumi bora.  Inavyoonekana Zari ambaye ni mjasiriamali kutoka nchini Uganda, mwenye makazi yake jijini Pretoria, Afrika Kusini, hayupo vizuri baada ya juzi kumbwatukia mmoja wa wafuasi wake mtandaoni.

Zari ambaye ni mzazi mwenza wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ alimwambia mfuasi wake huyo kwamba, yule aliyedai ni mumewe aliyefunga naye ndoa miezi kadhaa iliyopita, King Bae au Mr M, eti amekufa.

Zari ambaye ni mama wa watoto watano, alijikuta akitoa kauli hiyo baada ya mfuasi wake huyo kumuuliza mbona siku hizi King Bae haonekani? “Amekufa.” Zari alimjibu kwa kifupi. Majibu ya Zari yanaonekana kama alikuwa anatania, lakini baadhi ya wachangiaji kwenye ukurasa wake wa Instagram walihitimisha kwamba, kuna kitu hakijakaa sawa kwenye suala zima la uhusiano wa kimapenzi kwa Zari.

Baadhi ya watu walikwenda mbali na kudai kwamba, eti hakukuwa na King Bae, bali ilikuwa ni zuga tu baada ya kuachana na Diamond au Mondi ili naye aonekane wanaume wanamtaka. Wengine walidai kuwa, huenda alikuwepo mwanaume huyo, lakini sasa wameachana. Pamoja na kujulikana kuwa ana mwanaume aliyemtambulisha kwa jina hilo, lakini hakuwahi kumfunua au kumuonesha uso kwa madai ya kwamba anahofia nyakunyaku wa mjini watamuibia

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Pole mama huyu. wa pili anafariki
    ndiyo mana Domo kashtukia, w..zimepiga
    shoti..? Au ndiyo...

    ReplyDelete

Top Post Ad