Mbaroni kujifanya ofisa TAKUKURU

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(Takukuru) Mkoa wa Ilala, inamshikilia Mkazi wa Mbagala, Kijiji Dar es Salaam Hussein Mhando kwa kujifanya ofisa wa Taasisi hiyo.

Akizungumza na waandishi wa Habari’ leo Desemba 19, mwaka huu, Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Ilala, Christopher Myava amesema mtuhumiwa hiyo amegushi na kutengeneza kitambulisho namba PCCB 1565 chenye cheo cha Ofisa Mchunguzi Mkuu(principal investigator) .

Amesema kwa kutumia kitambulisho hicho mtuhumiwa amekuwa akiwatapeli watu na kujipatia kipato kinyume Cha sheria.

“Baada ya kupata taarifa Desemba 12, mwaka huu tulimwekea mtego Mwananyamala, kwa bahati mbaya alikimbia baada ya kuona watu asiowajua na kutelekeza gari lenye namba T618DMS alikitumia siku hiyo.

Amesema Takukuru ililishikilia gari hilo hadi Desemba 16 ambapo mtuhumiwa aliamua kujisalimisha na kukiri kutenda kosa hilo. 

Myava ametoa rai kwa wananchi kutoa taarifa kwa namba 113 pindi wanapobaini kuwapo kwa uhalifu wenye taswira ya rushwa.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad