Muuaji sugu wa Thailand Atambuliwa kwa Jeraha Alilokuwa Nalo

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Wanandoa wamemtambua mtu mwenye visa vingi vya mauaji Thailand, alipokuwa kwenye treni kwasababu ya jeraha alilokuwa nalo kwenye paji lake la uso na kukamatwa na polisi.

Somkid Pumpuang, 55, aliachiliwa mapema mwezi Mei, wakati akihudumia kifungo cha maisha kwa makosa ya mauaji ya watu watano.

Hatahivyo, alirejeshwa katika orodha ya watu wanaotafutwa na polisi baada ya kushukiwa kumuua mtu mwengine wa sita eneo la Kon Kaehn Jumapili iliyopita.

Polisi huko Thailand walianzisha msako dhidi yake baada ya mauaji ya hivi karibuni ya mwanamke mwenye umri wa miaka 51, Ratsami Mulichan.

Wanandoa hao vijana, ambao hawakutajwa kwasababu za kiusalama, walikuwa wameketi mkabala na Somkid walipokuwa kwenye treni saa 08:37 Jumatano asubuhi.

Mchumba wa kike ambaye alikuwa mwanafunzi alimtambua Somkid kwa jeraha kubwa alilokuwa nalo sehemu ya nyusi ya jicho la kushoto, ambalo lilikuwa sawa na lile la kwenye picha iliyotolewa katika orodha ya wanaotafutwa na polisi.

Wachumba hao waliondoka sehemu waliokuwa wameketi na kwenda sehemu nyengine lakini mchumba wa kike akamueleza mwenzie sababu zilizokuwa zinamtia wasiwasi, kisha akarejea tena sehemu aliyokuwa ameketi awali na kumpiga mhalifu huyo picha kisha akaituma katika kituo cha polisi.

Treni hiyo ilipowasili katika kituo kinachofuata cha Pak Chong saa 10:45, maafisa wa usalama walikuwa wameshawasili na moja kwa moja wakaingia katika behewa alilokuwa Somkid na kumkamata.

Mchumba wa kike alisema kwamba jeraha hilo "lilimthibitishia kwamba huyo ni Somkid", ameiambia Televisheni ya Thailand.

Kabla ya kukamatwa, polisi walimtaja Somkid kama "mwanamume hatari".

Maafisa hao wanadai kwamba Somkid alimuomba urafiki Ratsami Mulichan katika mtandao wa Facebook kwa kujidai kuwa yeye ni mwanasheria na kumtembelea nyumbani kwake Disemba 2.

Wiki mbili baadaye, alipatikana nyumbani kwake akiwa amekufa, kulingana na gazeti la Bangkok Post.

Mwaka 2005 Somkid alishtakiwa kwa makosa ya mauaji ya watu watano.

Waathirika wote walikuwa wanawake ambao walikuwa ama waimbaji katika vilabu vya usiku au wakandaji wa mahotelini.

Mwaka 2012, mahakama ya rufaa ilimuhukumu Somkid kifungo cha maisha.

Hata hivyo, mwezi Mei mwaka huu alipewa kifungo cha nje baada ya kuonesha kwamba amerekebisha tabia alipokuwa gerezani.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad