Askari Aliyekabidhi Mwizi kwa Raia Apigwe na Kuuawa, Afukuzwa kazi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Jeshi la polisi Zanzinzibar limemfukuza kazi askari polisi Hussein Yahaya Rashid (36) baada ya kumtia hatiani kwa kosa la kusababisha kifo cha Mussa Suleiman ambaye alituhumiwa kwa kosa la wizi.

Kamanda wa polisi mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, Awadh Juma Mohamed amethibitisha kufukuzwa kwa askari polisi huyo mwenye namba 3307412 ambaye mwezi Novemba mwaka jana alimkabidhi mtuhumiwa wa kosa la wizi kwa raia ambao walimshambulia hadi kusababisha kifo chake.


Kamanda Mohamed amesema askari huyo alitakiwa kumkabidhi mtuhumiwa kwa jeshi la polisi au kituo chochote kile ili kupata hifadhi na kusubiri taratibu nyingine za upelelezi pamoja na kufunguliwa mashtaka.

“Ni kweli Jeshi la polisi limemfukuza kazi aliyekuwa askari wake, Hussein Yahaya ambaye alimkamata raia anayetuhumiwa kwa makosa ya wizi, sasa yeye badala ya kumpeleka katika kituo cha polisi alimsalimisha kwa raia wenye hasira nakusababisha kifo chake” amefafanua kamanda Mohamed.

Na kuwataka askari wengine wa jeshi la polisi kuzifahamu sheria zinazoliongoza jeshi hilo ambalo linafanya kazi zake kwa ushirikiano mkubwa na raia.

“Jeshi la polisi kazi yake kubwa ni kulinda usalama wa raia, maisha yao na mali zao, huwezi kumkamata mtuhumiwa wa kosa la wizi na kumpeleka kwa raia wenye hasira na kumuua” amesisitiza kamanda Mohamed.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad