AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Mhubiri Elisha Misiko wa kanisa la Ground for Jesus, lililoko mjini Mombasa nchini Kenya, amemuua mke wake kwa kumchoma na kisu na kisha yeye kujikata koo lake na kufariki papo hapo, wakati wa ibada ya Jumapili ikiendelea kanisani hapo.
Tukio hilo limetoa leo Januari 5, 2020, ambapo kwa mujibu wa waumini wa kanisa hilo wamesema kuwa mhubiri huyo alitekeleza unyama huo kwa haraka sana na kwamba juhudi za kuwanusuru wawili hao hazikuzaa matunda.
Kwa upande wake Kamanda wa Polisi wa eneo la Kisauni, Julius Kiragu, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo lililotokea majira ya saa 4:00 asubuhi ya leo na kwamba Jeshi la Polisi mjini Mombasa, limekwishaanza kufanya uchunguzi ili kubaini nini chanzo kilichopelekea mume kumuua mkewe na kisha yeye naye kujikata koromeo.
Aidha Kamanda Kiragu amesema kuwa ndani ya mfuko wa suruali wa mhubiri huyo wakati wakiondoa mwili wake na kuupeleka katika chumba cha kuhifadhia maiti, wamekuta barua yenye kurasa 17, iliyokuwa ikieleza chanzo cha mauaji hayo kuwa ni migogoro ya kifamilia.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Migogoro ya kifamilia!! Ndio unaua?!? Ni roho chafu, asiige mtu, ni ya kukemea na kufanyia toba.
ReplyDelete