Gavana Atangaza Mapumziko Siku ya Kumpokea Rais Nigeria

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


 Uongozi wa jimbo la Ondo nchini Nigeria umetangaza kuwa kesho ni siku ya mapumziko, ambapo Rais Muhammadu Buhari wa nchi hiyo atakua na ziara katika jimbo hilo.

Gavana wa jimbo hilo la Ondo, Arakunrin Akeredolu amemualika Rais Buhari kufanya ziara katika jimbo hilo ambapo pamoja na mambo mengine atazindua miradi mbalimbali ikiwa ni sehemu ya sherehe za kutimiza miaka mitatu tangu Gavana huyo aingie madarakani.

 Akeredolu ametangaza kuwa Wafanyakazi wote katika jimbo hilo kesho hawatakwenda kazini, ili wapate nafasi ya kumpokea Rais Buhari na kushiriki kwenye sherehe hizo.

Sherehe hizo za kutimiza miaka mitatu madarakani kwa Gavana wa jimbo la Ondo, zilianza tarehe 21 mwezi huu na zinatarajiwa kufikia tamati Machi Mosi mwaka huu.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad