Tahadhari Kwa Waishio Pembezoni Mwa Mikondo Ya Maji Ya Bwawa La Mtera Na Kidatu

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



TAARIFA YA TAHADHARI KWA WANANCHI WANAOISHI PEMBEZONI MWA MKONDO WA MAJI YATOKAYO KWENYE VYANZO VYA KUFUA UMEME KWA MAJI VYA MTERA NA KIDATU

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linatoa taarifa kuwa kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha bwawa la Mtera limejaa kwa kiwango cha juu na kina cha maji kimepanda hadi kufikia mita 698.50 juu ya usawa wa bahari na hivyo kulazimu ziada inayoendelea kuingia kuanza kutolewa kupitia milango mahususi kuanzia  Februari 15, 2020 kwa ajili ya usalama wa Mabwawa na Mitambo.

Aidha, wastani wa mita za ujazo 1,200 kwa sekunde kinaendelea kutiririka bwawani.

TANESCO inaendelea kutoa tahadhari kwa Wananchi hususani wale wanaojishughulisha na shughuli mbalimbali za kiuchumi kama vile Uvuvi, kulisha Mifugo, Kilimo na shughuli nyingine kwenye mkondo wa mto, vidimbwi au pembezoni mwa bwawa kuacha kufanya shughuli za kibinadamu, kijamii na kiuchumi kwa kipindi hiki ambacho mvua za Vuli zikiwa zinaendelea kunyesha.

TANESCO itaendelea kutoa taarifa kadri hali ya kuruhusu ziada ya maji kupita upande wa pili itakavyokuwa inaendelea.

Imetolewa na: Ofisi ya Uhusiano
TANESCO-Makao Makuu
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad