AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
NAHODHA na kiungo wa Yanga, Papy Tshishimbi raia wa DR Congo, ni kama amemuachia msala kocha wa timu hiyo, Mbelgiji Luc Eymael akisema kwamba sare mfululizo wanazozipata kocha wao huyo ataweka mambo sawa na kurudi katika hali ya kushinda.
Yanga katika mechi tatu zilizopita kwenye Ligi Kuu Bara, imeambulia pointi tatu kwa kutoka sare zote dhidi ya Mbeya City, Prisons na Polisi Tanzania. Kwa sasa Yanga wana pointi 40 wakiachwa pointi 19 na vinara Simba wenye 59.
“Najua hizi sare ambazo tunapata ni changamoto za kimpira ambapo zitakaa sawa na tutarudi katika kasi yetu kama ambayo tumekuwa nayo.
“Naamini kocha (Eymael) na viongozi watakaa na kulitatua hili lakini pia sisi tunajiandaa na mechi yetu ijayo dhidi ya Coastal Union kuona tunapata matokeo ambayo yatakuwa mazuri,” alisema Tshishimbi.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK