Mbowe Aeleza Mwanaye Alivyopata Corona "Hatustahili Kuchefuliwa na Kejeli za Makonda"

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe amemuomba Rais Magufuli, kushirikisha wadau wengine nje ya Serikali ili kwa pamoja waweze kukabiliana na janga la Corona kwa kuwa lipo mlangoni kwa kila mtu kwani hata mwanaye umempata ndani ya nchi.

Mbowe aliyasema hayo kupitia taarifa ya familia yake kwa umma na Dunia nzima, wakati akieleza ni kwa namna gani mwanaye alivyopatwa na maambukizi ya Virusi vya Corona, ambapo amesema huu si wakati wa malumbano na njia pekee ya kulishinda janga hilo ni kulikubali na kulikabili.

"Hali ya Dudley sasa imeimarika, homa zimekwisha, bado yuko chini ya uangalizi maalum kwenye karantini, hatustahili kuchefuliwa na kejeli za Makonda, Rais wetu John Magufuli, unda timu ya kukusaidia na ushirikishe wadau wengine, wengi wako tayari kukusaidia CHADEMA tuko tayari kukusaidia na kulisaidia Taifa, siyo wakati wa kulumbana  huu" amesema Mbowe.

Aidha Mbowe ameongeza kuwa katika maisha, maandalizi hayajawahi kuwa hasara, bali hasara iliyo majuto ni kutokujiandaa na kupuuza yanayofanywa na walioyapitia kama zilivyo nchi zingine zilizoendelea.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad