AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
RAIS wa Urusi, Vladimir Putin, kuanzia sasa atakuwa akifanya kazi akiwa nyumbani kwake huko Novo-Ogarevo, karibu na jiji la Moscow, msemaji wa Kremlin amesema siku moja baada ya daktari aliyekutana na rais huyo wiki iliyopita kupatikana na virusi vya Corona.
Kiongozi huyo wa Urusi anatarajiwa leo mchana kuongoza mkutano wa wajumbe wa serikali yake kwa njia ya video, Dmitry Peskov amewaambia waandishi wa habari, akibainisha kwamba Putin, ambaye kwa mujibu wa Kremlin yuko katika afya njema, sasa ameamua kufanya kazi akiwa nyumbani kwake.
“Kila mtu sasa anajitenga na wengine kutokana na hali inayojiri kwa sasa,” Peskov ameongeza.
Visa 2,777 vya maambukizi ya virusi vya Corona vimethibitishwa nchini Urusi ambapo watu 24 wamefariki dunia kwa ugonjwa huo ambao ulianzia nchini China mwezi Desemba mwaka 2019, kabla ya kusambaa katika zaidi ya nchi 200 kote ulimwenguni.
Katika kujaribu kukabiliana na kuenea kwa virusi hivyo, hasa katika mji mkuu, ambao umekuwa kitovu cha janga hilo nchini humo, siku ya Jumapili Manispaa ya Jiji la Moscow ilitangaza marufuku kwa watu kutoka nje ya makazi yao.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK