Chadema Wadai Kutostushwa na Madiwani wao Kutimkia CCM

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Na Amiri kilagalila,Njombe

Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA mkoa wa Njombe kimesema hakijashtushwa na taarifa za Madiwani wao watatu wa wilaya ya Makete kutangaza kuhamia Chama cha Mapinduzi CCM kwa kuwa walishakuwa na taarifa za kuwa wamekuwa wakitishwa kwa muda mrefu.

Mwenyekiti wa CHADEMA mkoa wa Njombe Rose Mayemba amesema kuwa licha ya madiwani hao kutotoa sababu hizo hadharani lakini kama chama kilishapata taarifa hizo kwa muda mrefu kwamba wamekuwa wakitishiwa mara kadhaa na kuwataka kuachana na chama hicho.

“Taarifa za kuhama kwa madiwani wetu 3 wilayani Makete,kama chama hatujastushwa kwasababu tulishakuwa na taarifa za awali na tulijaribu kuhojiana nao na wengi wao walisema kabisa namna ambavyo wanatishwa na kuhatarishiwa maisha yao na wakaona hawawezi kustahimili na wakaamua kuondoka kwa hiyo haijatustua na tulishaifuatilia” amesema Rose Mayemba mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Njombe                 

Hata hivyo bado kumekuwapo kwa taarifa za muda mrefu kuwa kuna baadhi ya madiwani wao katika majimbo mengine likiwemo la Njombe Mjini kuwa wanampango wa kuhamia CCM wakati wowote Mwenyekiti huyo wa Chadema amesema tayari wameshakaa nao licha ya kukataa.

“Hata hao wengine tunafahamu na tumezungumza nao ila wengine wanakataa na wengine wanakiri kwamba CCM wanawafuata na kuwatisha lakini sisi kama chama tunawaonya CCM sio tabia njema kwa ustawi mzuri wa demokrasia,wananchi walitakiwa kuacha huru kila mmoja asimame mahali ambapo kwake ni sahihi japo kuwa pia ni haki ya kikatiba mtu kutoka”alisema tena Rose Mayemba

Agrey mtambo ni katibu wa madiwani mkoa wa Njombe na diwani wa kata ya Njombe Mjini ambaye anasema licha ya kuwa madiwani hao wamehama Chadema kwa mujibu wa katiba lakini wanashangazwa na kitendo hicho kufanyika ikiwa imebaki mwezi mmoja kumaliza muda wao jambo linalowakosesha stahiki zao za udiwani.

“Tumebakiwa na mwezi mmoja tu kustaafu lakini Yule aliyetumika mpaka mwezi wa jana na kuhamia chama kingine tafsiri yake sio mwanachama wa Chadema,taratibu za kimaslahi binafsi zitakuwaje hatujui”alisema Mtambo

hata hivyo diwani mtambo amekanusha taarifa za kuwa baadhi ya madiwani wanampango wa kuhama chama hicho na kutimkia ccm.

Madiwani hao watatu wa makete waliotimkia CCM hivi karibuni ni  pamoja na Asifiwe Luvanda aliyekuwa diwani wa kata ya Iwawa,Betrece Kyando aliyekuwa diwani wa viti maalum kutoka tarafa ya Lupalilo na Efati Mbogela Mwipelele aliyekuwa diwani wa kata ya Ipelele ambao wamesema wamehamia CCM bila shinikizo toka kwa mtu yeyote.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad