AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Wabunge 21 na madiwani 09 wa CUF,waliomaliza muda wao, wakiongozwa na Ally Salehe, Mbunge wa Malindi Visiwani Zanzibar, kumejiunga na ACT-Wazalendo.
Wabunge hao wastaafu wamepokelewa leo Jumamosi tarehe 20 Juni 2020 jijini Dar es Salaam, na viongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, akiwemo Maalim Seif Sharrif Hamad, Mwenyekiti wake na Zitto Kabwe, Kiongozi wa chama hicho.
Wimbi la wanachama wa CUF kutimkia ACT-Wazalendo ,limeshika kasi tangu mwezi Machi mwaka 2019, baada ya kuibuka kwa mgogoro wa kiuongozi baina ya Maalim Seif , aliyekuwa Katibu Mkuu wa chama hicho, na Prof. Ibrahim Lipumba, Mwenyekiti wa CUF.
Akizungumza kwa niaba ya wabunge hao, Salehe amesema wamejiunga na chama hicho baada ya kuona CUF imepoteza nguvu ya kuhimiri vishindo vya siasa
Salehe amesema wanaanza upya ndani ya ACT-Wazalendo, huku akijigamba kwamba wamejipanga kutetea majimbo yao kwenye Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2020.
Aidha, Salehe amesema walitamani kujiunga na ACT-Wazalendo pamoja na Maalim Seif na wafuasi wake kupitia kampeni ya ‘Shusha Tanga, Pandisha Tanga’, lakini walishindwa kutokana na sababu zilizookuwa nje ya uwezo wao.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK