AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Wakili wa Kujitegemea, Fatma Karume achekelea taarifa ya kutumbuliwa kwa viongozi watatu wa Mkoa wa Arusha akiwemo Mkuu wa Mkoa huo, Mrisho Gambo.
Mbali na kicheko hicho Fatma alirusha kijembe katika ukurasa wake wa Twitter huku akiweka ujumbe huu ” Wakati wa uchaguzi matongotongo yanatoka machoni ubaya unaonekana,” aliandika ujumbe huo.
Rais John Magufuli amewatumbua viongozi watatu wa mkoa wa Arusha akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo kwa vyombo vya habari na Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Gerson Msigwa, imeeleza kuwa Rais Magufuli amefanya uteuzi wa viongozi wengine watakaoshika nyadhifa hizo.
Rais Magufuli amemteuwa Idd Kimanta kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha. Kabla ya uteuzi huo Kimanta alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Monduli mkoani Arusha na kwamba nafasi hiyo ya Mkuu wa Wilaya ya Monduli itajazwa baadaye.
Aidha, Rais Magufuli ametengua uteuzi wa Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Gabriel Daqarro na amemteua Kenan Kihongosi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Arusha.
Kabla ya uteuzi huo Kihongosi alikuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Iringa.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Shangazi. Si uliwahi kuwa wakili zamani kabla ya kukushindwa kazi..!! Nasikia umeanzisha duka LA fesheni huko Ungonini.
ReplyDeleteHivi wewe wa Wapi?? Karibu nyumbani Tandahimba uone Babu na bibi WA babu. Kuna kolosho tu. Tena msimu huu zimezaa mpaka utapenda. Cameliusi alikuwa anakuongelea hivi punde. Tuna kumissi na koti jeusi kama zamani. Umeisikia Ofa ya DC