"Wanaobeza Uchumi wa Kati ni Wagonjwa" - Pinda

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Waziri Mkuu Mstaafu Mizengo Pinda, amempongeza Rais Magufuli pamoja na Watanzania kiujumla, kufuatia ripoti ya Benki ya Dunia iliyoitaja Tanzania kama imefikia kuwa nchi yenye uchumi wa kati na kuwashangaa wale wote wanaobeza hatua hiyo na kudai kuwa ni wagonjwa wa akili.


Kauli hiyo ameitoa hii leo Julai 12, 2020, wakati akizungumza kwenye hafla fupi iliyoandaliwa na Rais Magufuli Ikulu ya Chamwino Dodoma, ambayo aliwaalika Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM), kwa ajili ya kupata chakula cha mchana.

"Mh Rais naomba niseme kwa dhati nikupongeze wewe pamoja na Watanzania kiujumla, kutokana na ile taarifa ya Benki ya Dunia ya kwamba Tanzania imeingia kwenye uchumi wa kati, si jambo dogo naona kwenye mitandao wanabeza na mimi nikasema nadhani ni wagonjwa wa akili, tumetoka katika ile hatua ambayo tulikuwa tunatazamwa kama nchi maskini" amesema Waziri Mstaafu.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad