Barbara Awachimba Mkwara Mzito Yanga

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA





Mtendaji Mkuu (C.E.O) wa Simba, Barbara Gonzalez.

WAKATI wakiwa wanatarajia kukutana kwenye fainali ya Kombe la Shirikisho (FA), Mtendaji Mkuu (C.E.O) wa Simba, Barbara Gonzalez ni kama ametuma ujumbe mzito kwa wapinzani wao Yanga kwa kubainisha wazi kwamba watachukua ubingwa huo.

 

Mtendaji huyo ameongeza kwamba licha ya ugumu wa kukabiliana na watani zao hao lakini mipango yao ni kulibeba taji hilo sambamba na ubingwa wa ligi kuu.



Simba na Yanga zote zimepenya fainali ya FA baada ya kushinda mechi zao za nusu fainali kwa bao 1-0 kila moja, Simba wakishinda mbele ya Azam FC na Yanga wakiwachapa Biashara United.

 

Barbara amesema kwamba licha ya ugumu ambao wanao wapinzani wao wote kwenye ligi lakini hesabu zao ni kuhakikisha kuwa wanachukua mataji hayo mawili mwisho wa msimu.

 

“Mashabiki wetu tunawaomba watuombee hasa kwenye mechi hizo mbili, ya ligi na FA. Mechi zote ni ngumu kwa sababu hakuna timu rahisi kwenye ligi kuu lakini tuko tayari kupambana, tulisema mwanzo wa msimu kwamba tunahitaji vikombe vyote kwenye FA na ligi kuu.”

Stori na Said Ally,Dar es Salaam

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad