Kapombe atajwa tena Tuzo ya mashabiki Simba SC

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Beki wa kulia Shomari Salum Kapombe ametajwa tena kwenye orodha wa wachezaji wanaowania tuzo ya mchezaji bora wa mwezi Machi Mabingwa wa Soka Tanzania Bara Simba SC.


Kapombe alitangazwa kuwa mshindi wa tuzo hiyo mwezi uliopita akiwashinda Kiungo Mshambuliaji kutoka Malawi Peter Banda na Beki kutoka DR Congo Henock Inonga.


Kwa Mwezi huu Machi Kampombe anashindanishwa na Kiungo Mshambuliaji kutoka nchini Malawi na Pape Sakho (Kiungo Mshambuliaji kutoka nchini Senegal).


Simba SC imetoa orodha hiyo leo Jumatano (Machi 23), ambapo mashabiki wa klabu hiyo wataanza kupiga kura na baadae mshindi atatangazwa kupitia kurasa za Mitandao ya Kijamii za Mabingwa hao wa Tanzania Bara. Mbali na Kapombe kutwaa tuzo ya Mchezaji Bora wa Simba SC mwezi Februari, Pape Ousman Sakho alitangazwa kuwa mshindi wa mwezi Januari, huku Kiungo Jonas Mkude akiibuka kidedea mwezi Desemba 2021.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad