Meli Iliyobeba Magari Ya Kifahari 4,000 Yazama Ureno

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Meli ya mizigo iliyokuwa imebeba magari ya kifahari takribani 4,000, imezama katika Visiwa vya Azores nchini Ureno, zikiwa zimepita wiki mbili tangu iliposhika moto.

Meli hiyo iitwayo Felicity Ace, ilikuwa ikisafirisha magari hayo ya kifahari, yakiwemo aina ya Porsches na Bentleys na ilikuwa njiani kuelekea Kisiwa cha Rhode nchini Marekani kutokea bandari ya Ujerumani ya Emden wakati moto ulipozuka.

Wahudumu wote wa meli hiyo waliokolewa wakati moto huo ulipoanza Februari 16.





Joao Mendes Cabecas, nahodha katika moja ya bandari iliyo karibu katika Kisiwa cha Faial, ameliambia Shirika la Habari la Reuters kwamba hakuna uvujaji wa mafuta ulioripotiwa hadi sasa lakini amesema kuna hofu kwamba matenki ya mafuta yanaweza kuharibika wakati chombo hicho kikiwa chini ya Bahari ya Atlantic, katika kina cha mita 3,500.

Jeshi la wanamaji la Ureno limesema hakuna aliyejeruhiwa na moto huo na kwamba wafanyakazi wote 22 wa meli hiyo walipelekwa katika hoteli moja baada ya jeshi la wanamaji, meli nne za wafanyabiashara waliokuwa wakisafiri katika eneo hilo na Jeshi la Anga la Ureno kukamilisha zoezi hilo la kuwokoa.


Kampuni ya kutengeneza magari ya Volkswagen imesema uharibifu wa magari hayo yenye bima unaweza kugharimu karibu dola milioni 155 kwa mujibu wa Shirika la Habari la Reuters.


Kampuni ya Bentley ilithibitisha kuwa magari yake 189 yalikuwa ndani ya meli hiyo na kampuni ya Porsche ilisema ilikuwa na magari 1,100 katika meli hiyo.

Mteja mmoja alituma ujumbe wa Twitter akisema kuwa Porsche yake ilikuwa kwenye meli iliyoteketea. Mwingine alituma ujumbe wa Twitter kwamba alikuwa amerudishwa nyuma.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad