Simon Msuva Azikana Timu za Bongo "Kucheza Simba au Young Africans HAPANA

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Hatimaye Kiungo Mshambuliaji wa Tanzania Simon Msuva amekanusha taarifa za kuwa mbioni kurejea katika Soka la Bongo huku akihusishwa na klabu nguli za Simba SC na Young Africans.

Msuva aliingia kwenye fununu za usajili wa klabu hizo kongwe katika Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati, kufuatia sakata lake la kimaslahi dhidi ya Uongozi wa Wydad Casablanca ya Morocco, hali ambayo inatazamwa huenda ikavunja mkataba wa pande hizo mbili.

Baada ya mchezo wa Taifa Stars dhidi ya Jamhuri ya Afrika ya Kati uliochezwa jana Jumatano (Machi 24) Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es salaam, Kiungo huyo alizungumza na Waandishi wa Habari na kusema hafikirii kujiunga na klabu za Tanzania na badala yake amejikita kwenye wazo la kuendelea kucheza soka nje ya nchi.

“Kuna klabu nyingi zimeshaonyesha nia ya kutaka kunisajili katika kipindi hiki, lakini sina budi kusubiri hadi sakata langu la Wydad litakapokwisha.”


“Kwa Tanzania hapana.” amesema Msuva

Tayari Shirikisho la Soka Dunia FIFA limeshapokea malalamiko ya Simon Msuva dhidi ya Wydad Casablanca, na wakati wowote maamuzi ya kesi hiyo yatatangazwa.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad