Bernard Morrison Aomba Jezi 100 za Simba SC Kugawa Nchini Kwao Ghana

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kiungo Mshambuliaji kutoka nchini Ghana Bernard Morrison ameonesha bado ana mapenzi na Klabu ya Simba SC, licha ya kuhusishwa na mpango wa kusajiliwa na Mabingwa wa Soka Tanzania Bara Young Africans.


Morrison anatajwa kukamilisha dili la kurejea Young Africans, kufuatia mkataba wake na Simba SC kutarajia kufikia kikomo Agosti 30, huku Uongozi wa Msimbazi ukimpa mapumziko hadi mwishoni mwa msimu huu 2021/22.


Kiungo huyo ambaye amekua kivutio cha wadau wengi wa soka Tanzania kutokana na vibweka vyake, amedhihirisha bado anaipenda Simba SC, kufuatia ujumbe aliouandika kwenye ukurasa wake wa Instagram, akiomba mchango wa manunuzi ya jezi za klabu hiyo.


Morrison anaomba msaada huo kwa ajili ya kuzigawa kwa Mashabiki na Familia nchini kwao Ghana.


Morrison ameandika: Mara nyingi tunakatishwa tamaa na wale tunaowapenda na kuwaamini. Lakini wacha nifanye hadithi yangu kuwa fupi na rahisi, nahitaji jezi 100 za Simba SC kutoka kwa mashabiki waaminifu kwa ajili ya marafiki na familia nchini Ghana. 


Hii ni kutokana na nyinyi mashabiki kuniaga kwa sababu nitakatishwa tamaa ikiwa nitaendelea kusubiri kupata moja kutoka kwa klabu yangu.  tafadhali andika jina lako nyuma na namba 3.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad